Posts

DKT. KIJAJI: USHINDI WA TUZO ZA UTALII DUNIANI NI MATUNDA YA FILAMU YA “TANZANIA: THE ROYAL TOUR”.

Image
Na Philipo Hassan – Dodoma Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) ameeleza kuwa Tanzania kuibuka mshindi wa Tuzo mbalimbali za utalii duniani ni matunda ya filamu ya “Tanzania: The Royal Tour” iliyochezwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Waziri Dkt. Kijaji amesema hayo leo Desemba 15, 2025 katika hafla ya kupokea na kusherehekea tuzo za kimataifa ambazo Tanzania imeshinda katika sekta ya utalii kwa mwaka 2025. Hafla hiyo imefanyika katika Ofisi za Wizara ya Maliasili na Utalii, Mtumba Jijini Dodoma. “Tunautambua na kuuthamini kwa upekee mchango wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Filamu ya “Tanzania: The Royal Tour”. Hakika mafanikio haya ni jitihada zake mahsusi kwa yeye binafsi kufungua milango ya kutangaza utalii wa Tanzania kimataifa, ambapo leo hii tunashuhudia jumla ya tuzo 5 za utalii ambapo zimeendelea kuipeperusha bendera ya Tanzania duniani” ~ alieleza Dkt. Kijaji. Dkt. Kijaji aliongeza kuwa “Tanzania kuteuliwa...

KAIMU KAMISHNA WA UHIFADHI TAWA AFUNGUA KIKAO KAZI CHA MENEJIMENTI YA TAWA

Image
Na. Mwandishi wetu, Mwanza. Kaimu Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA, Mlage Yussuf Kabange amefungua rasmi kikao kazi cha Menejimenti ya TAWA kilichofanyika Disemba 13,2025, katika ukumbi wa Malaika, jijini Mwanza. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao kazi hicho kilichojumuisha Makamishna Wasaidizi Waandamizi, Makamanda wa Kanda na Wakuu wa Vituo vyote vya TAWA, Kamishna Kabange amesema lengo kubwa la kikao hiki ni kuboresha utendaji kazi ili kufikia malengo ya Mamlaka. Kamishna Kabange ameibainisha kuwa kikao kazi hiki kitajikita katika vipaumbele mbalimbali vitakavyoboresha maeneo ya utendaji kazi wa TAWA yakiwemo maeneo ya ulinzi na usimamizi wa wanyamapori, ukusanyaji wa mapato, migongano baina ya binadamu na wanyamapori, ujenzi wa miundombinu katika hifadhi pamoja na kuboresha mazingira ya kazi hususan kwenye maeneo ambako askari wanafanya kazi. Sambamba na hilo, Kamishna Kabange amewasisitiza Makamishna Wasaidizi Waandamizi na Makamanda wa Kanda ku...

THE PUNISHMENT FOR ADULTERY AMONG THE HADZA COMMUNITY

Image
By Our Correspodent, Ngorongoro. The Hadza community, found along the shores of Lake Eyasi in Karatu District, Arusha Region, is among the Indigenous groups living within the Ngorongoro–Lengai UNESCO Global Geopark. They are also beneficiaries of the new geological heritage museum situated in Karatu town. Across Tanzania, and Africa more broadly, many communities uphold longstanding customs and regulations designed to preserve their traditions, values and social order. Among the Hadza (also known as the Watindiga), adultery is considered a severe offence. When a married man or woman engages in sexual relations outside the marriage, the act is viewed not only as a betrayal of trust but as a serious curse upon the family and the wider community. According to Hadza tradition, once such an offence is verified, the individuals involved may be killed by the person who caught them in the act. After carrying out the killing, the witness issues a loud call to alert the community, at which point...

Zanzibar Leads Africa in Corporate Retreat Excellence – 2025 Awards

Image
                                      By Philipo Hassan  Zanzibar has once again affirmed its position as a premier business and leisure destination after being recognized as Africa’s Best Corporate Retreat Destination 2025 at the prestigious World MICE Awards. This global recognition highlights Zanzibar’s growing influence as a top hub for Meetings, Incentives, Conferences, and Exhibitions (MICE), offering world-class facilities, pristine island environments, and exceptional hospitality services that cater to both business travelers and high-end retreat seekers. The 2025 World MICE Awards brought together leading destinations, organizations, and industry professionals from around the world. Zanzibar stood out for its outstanding performance in delivering unique corporate retreat experiences—perfect for strategic meetings, executive team-building, incentive travel, and luxury business esc...

KAMISHNA KUJI: AHIMIZA WATUMISHI KUJIENDELEZA KIELIMU ILI KUBORESHA UFANISI KATIKA UTENDAJI

Image
Na. Philipo Hassan - Arusha  Kamishna wa Uhifadhi Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), CPA Musa Nassoro Kuji, amewataka Maafisa na Askari Uhifadhi wa Uhifadhi waliopo TANAPA Makao Makuu na Kanda ya Kaskazini kujiendeleza kielimu ili kuboresha ufanisi katika utendaji kazi. Aliyasema hayo leo Julai 16, 2025, alipofanya kikao kazi cha Maafisa na Askari waliopo TANAPA Makao Makuu na Kanda ya Kaskazini, kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Kibo uliopo katika eneo la Makao Makuu ya TANAPA katika Jengo la Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu Jijini Arusha. Akizungumza katika kikao hicho, Kamishna Kuji alieleza umuhimu wa kujiendeleza kielimu, jambo ambalo linasaidia kuongeza ujuzi, maarifa ya kukabiliana na changamoto zinapojitokeza, kuboresha huduma nyakati za kuwahudumia watalii na kuwa wabunifu ili kuleta ufanisi mahali pa kazi. “Katika utendaji wenu wa kila siku kama watumishi wa TANAPA, tunategemea sana maarifa na weledi wenu ili kuboresha utendaji kazi. Hivyo, k...

RAIS DKT. SAMIA: BARABARA MPYA YA TANGA, PANGANI, SAADANI NA BAGAMOYO KUIFUNGUA TANGA KIUTALII

Image
Na Philipo Hassan - Tanga Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alisema kuwa kukamilika kwa barabara ya lami inayounganisha Tanga, Pangani, Saadani na Bagamoyo pamoja na Daraja la Mto Pangani lenye urefu wa mita 525 zitasaidia kuifungua Tanga Kiutalii na kiuchumi. Rais Samia ameyasema hayo leo, Februari 26, 2025 wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi katika ujenzi wa  barabara na Daraja la Mto Pangani ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa ziara yake mkoani Tanga. Vilevile, alisisitiza kuwa miundombinu hiyo mipya itarahisisha maeneo mengi ya utalii kufikika kiurahisi. Rais Samia alieleza “Barabara hii tunayoiunganisha inaenda kuifungua Tanga kiutalii na kibiashara. Maeneo mbalimbali ya kiutalii ambayo hayafikiki, itakuwa ni rahisi kumtoa mtalii Hifadhi ya Taifa Saadani na kwenda kutalii maeneo mengine ndani ya Mkoa wa Tanga”  Naye, Mbunge wa jimbo la Pangani Mhe. Jumaa Aweso alimshukuru Rais Samia kwa kutekeleza mradi mkubwa wa barabara na Daraja ambayo yat...

SIX RIVER AFRICA NA ECO WASHIRIKIANA NA TANAPA KUBORESHA HUDUMA ZA MATIBABU YA WANYAMAPORI

Image
Na. Happiness Sam- Same Shirika la Six Rivers Africa pamoja na Elephant Conservation Organisation (ECO) yameungana na TANAPA ili kuimarisha huduma za matibabu ya wanyamapori katika hifadhi za kanda ya kaskazini kwa kuongeza vitendea kazi ikiwemo gari, vifaa tiba pamoja na dawa za kutibu wanyamapori ili kuhakikisha ustawi wa wanyamapori unaimarika katika maeneo hayo. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Mradi wa Tiba ya Wanyamapori, jana Februari 18, 2025 katika Hifadhi ya Taifa Mkomazi iliyopo Wilaya ya Same, Mkoani Kilimanjaro, Mkuu wa wilaya ya Same Kasilda Mgeni alieleza umuhimu wa uhifadhi kwa maendeleo ya taifa kwani unasaidia katika kutunza urithi wetu wa asili ikiwemo wanyamapori kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vizazi vijavyo. DC Mgeni alisema  “Mradi wa Tiba ya Wanyamapori (Veterinary Support Project) ulianzishwa mwaka 2013 katika Hifadhi yetu ya Taifa ya Mkomazi kwa lengo la kuchukua hatua muhimu katika kuhakikisha mafanikio endelevu ya juhudi zetu za uhifadhi, mradi ...